MKUTANO WA PROF.
MAGEMBE WAZIRI WA MAJI NUSURA ULETE BALAA KWA WANANCHI WA MJI WA MUGUMU
–SERENGETI.
05/05/2013.
Waziri wa maji Mhe. Prof. Jumanne Magembe akiwa katika
ziara ya Kiserikali ya kukagua miradi mbalimbali ya kimaendeleo hasa katika
sekta ya maji amefika leo katika wilaya ya Serengeti mkoani mara akiambatana na
mbunge wa jimbo la Serengeti Mhe. Dr. Steven Kebwe pamoja viongozi wengine toka
Sekretarienti ya maji toka wizarani. Pia Mhe. Magembe akiwa Serengeti
ameambatana na timu ya watalaam toka sekretarieti ya maji ya mkoa wa Mwanza na
viongozi toka Mamlaka ya maji safi na taka ya mkoa wa Mara ambao ndio wangalizi
wa mradi wa Bwawa la Manchira la wilaya Serengeti.
Baada ya waziri kutembelea Bwawa la wa Manchira kama
ilivyo kawaida kwa viongozi wa juu wa serikali kila wafikapo Serengeti huenda
kutembelea Bwawa hilo, majira ya saa 11 jioni aliwasili katika Mji wa Mugumu
kwa ajili ya kuongea na wananchi waliokuwa wakisubiria kusikia kauli yake
katika eneo la uwanja wa Mbuzi.
Kama ilivyo kawaida na desturi yetu watanzania, kabla
ya kiongozi husika kusimama na kuongea na wananchi basi kunakuwepo na salamu na
maneno ya hapa na pale toka kwa viongozi wenyeji na pengine wale walioambatana
na kiongozi mkubwa, hii yote ikiwa ni kutaka kuweka vizuri hali ya hewa kwa
maana ya kuandaa wananchi kumsikiliza kiongozi mkubwa pindi uadiapo mda wake wa
kuongea.
Leo katika eneo la
uwanja wa mbuzi ilikuwa hivi;
Kwanza kabisa
alianza katibu Tarafa ndg. Shanyangi kuwasalimia wananchi kwa kusema Serengeti
hoeeee! Wananchi hawkujibu chochote, tena akarudia salamu kama mara mbili mara
tatu hivi Serengeti hoeeeeeeee, Magembe Safiiiiiiiiii, wananchi kimya na badala
yake zilisikika sauti chache toka meza kuu sehemu walipoketi viongozi wa chama
na serekali pamoja na waziri mwenyewe zikisema safiiii. Na mwisho katibu huyo
alihoji mbona wananchi mnanyaza, kuna tatizo gani? Wananchi wakasema unalijua.
Baada ya hapo ndg.
Shanyangi alimwita Mbunge Viti maalum na katibu wa UWT –Taifa aliekuwa
ameambatana na waziri Magembe kuja kusalimia wananchi na kusema machache……pia
hali haikuwa nzuri kwa mama huyo kwani alijikuta akiongea huku wananchi wakiwa
na minongono ya hapa na pale, alijaribu kuwasihi hata kwa kutumia baadhi ya
maneno ya kilugha kwa kutoa salamu pia haikuweza kuzaa matunda vizuri, ambapo
mbunge huyu alijikita katika kuwambia wananchi kuwa kama wanangalia TV yeye ni
mchangiaji mzuri bungeni na katika Bunge hili linaloendelea yeye amechangia
mara 4 katika mambo mbalimbali ikiwemo kuwatetea wafanyakazi.
Baada ya katibu huyo alifatia kaimu Mkuu wa wilaya ya
Serengeti ndg. Joshua Mirumbe ambae pia kama kawaida aliaza kwa kuwasalimu
wananchi wa wilaya yake ne akambulia patupu lakini hakuishia hapo aliendelea
kusema machache ya moyoni mwake kwa wananchi wake na kuwaomba wamsikilize
waziri Magembe kwani amekuja na majibu ya matatizo yao hasa kero ya maji katika
mji wa Mugumu na vijiji jirani, na baada ya hotuba yake fupi alisema sasa
naenda kumwita Mbunge wa jimbo letu mhe. Kebwe hapo ndipo wananchi walianza kwa
kuzomea na kupiga kelele za hapa na pale kwa kukataa kutomsikiliza mbunge
wao………kwa kusema wooooooooh, hatutaki huyo hapanaaaaaaaa,
Baada ya kusikia maneno hayo Mkuu wa wilaya
alipandisha jazba na kusema “hamtaki nini? Huu ni mkutano wa serikali mnaleta
uhuni, hatutaki uhuni hapa, OCD nakwamuru simama na hakikisha wanaoleta uhuni
hapa wanathitiwa mara moja, Serekali inawatea majibu ya matatizo yao then wao
waleta upuuzi, alisema DC Mirumbe”. Na kwa kauli hiyo ya DC MIrumbe OCD alitoa
ishara kwa askari polisi waliokuepo eneo hilo na walianza kutanda kwa kuzingira
wananchi na wananchi waliokuepo walilazimika kuwa kimya na ndipo Mbunge alipo
simama na kuongea na kwa hali isiyo ya kawaida Mbunge alianza kuhutubia bila
kusalimiana na wananchi wake.
Mpka mwanablog hii anaondoka eneo hilo la mkutano,
waziri Magembe katika hotuba yeke kwa wanamugumu alisema serekali kupitia
wizara yake ya maji imetenga kiasi cha shilingi milioni mia tano
(500,000,000/=) katika bajeti ya serekali ya mwaka 2013/2014 kwa ajili ya mradi
wa usambazaji maji safi na salama toka bwawa la manchira Serengeti , ambapo
pesa hizo zinatarajiwa kutumika katika uwekaji wa tank la kuchunja na kutibu
maji toka Bwawani, huku watalaamu wakisema kuweka chujio linaghamu kiasi cha
Bil. 7, swali linabaki kuwa je hizi mil.500 za Magembe zitawasaidia wanasengeti
kuondokana na tatizo la kunywa maji yasio safi na salama?
Mwisho………..
Swali: kwa nini hawa wananchi wanakataa kumsikiliza
mbunge wao waliomchagua wenyewe?
Mpaka washurutishwe na mkuu wa wilaya?