TATIZO
LA MAJI MUGUMU/SERENGETI BADO NI KITENDAWILI.
Na Samwel M.P
03/09/2016
Ndivyo
tunavyoweza kusema kuwa tatizo hili la maji katika mji wa Mugumu na viunga
vyake kuwa sasa ni kitendawili amabacho kinahitaji kuteguliwa na mamlaka zote
husika kwa haraka ili kuwanusuru
wananchi na hatari ya milipuko ya magonjwa amabayo yanaweza kujitokeza kutokana
na kukosekana kwa huduma ya maji safi kwa ajili ya matumizi ya majumbani. Lakini
pia inavyoelekea kitendawili hiki kinaweza kisiteguliwe kwa wakati kama
hakutakuwepo na msukumo/shinikizo la kutoka kwa wananchi wenyewe ambao ndio
wahanga wa tatitizo hili kwa kusaidiwa na mwakilishi wao bungeni ambae ni
mbunge wa jimbo la Serengeti Mhe. Marwa Ryoba, Serengeti ONLINE imebaini.
Kwa mujibu
wa taarifa ya mhandisi wa maji wilaya, Eng. Marwa Mlaza, tatizo hili la
kukosekana kwa huduma ya maji kwa wananchi wa Mugumu, lilianza tangu tarehe
09/05/2016 ambapo pump ya kusukuma maji toka bwawa la manchira iliungua. Mchakato
wa kupata mkandarasi na kuwagiza pump mpya na motor chini ya mamlaka ya maji
Musoma –MUWASA ulifanika na hadi sasa zoezi hilo halijakamilika kutokana na
motor kungua mara mbili. Hivyo basi ifikapo tarehe 09/09/2016 itakuwa imekamilika
miezi 4 mfululizo sawa na siku 120 bila maji kwa wananchi na wakazi wa mji wa
Mugumu, jambo ambalo ni hatari kwa maisha ya binadamu na mazingira yake
vilevile.
Leo sept.
03, mwandishi wa blog hii ametembelea Manchira ambako kulitarajiwa kuwa na
zoezi la kufunga motor kwa ushirikiano wa watalaam toka wizara ya maji (Dsm),
MUWASA (Musoma), Supplier wa Motor (Arusha) na mafundi wa MUGUWASA na
H/Mashauri ya wilaya Serengeti; zoezi hili limeshindwa kufanyika na watu
kutawanyika kutokana na sababu zifuatazo kama ilivyoelezwa:-
1) Hapakuwepo na
mwakilishi au mtalam toka upande wa supplier wa motor kutoka arusha, na
alipotakiwa kutoa ithini ili mafundi wa wizara na MUWASA kuendelea na ufungaji
wa motor alikubali kwa maneno kupitia simu, na badae wakamuomba akubali kwa maandishi kupitia barua pepe (email) kama
sehemu ya kuweka kumbukumbu, mkandarasi alikataa na kusema wamsubiri hadi siku
ya jumatano Sept. 07 ndiyo anaweza kutuma
mafundi wake kuja Mugumu jambo ambalo pia linaweza kuwa sii la ukweli kama
ilivyodaiwa kuwa amekuwa akiahidi uongo mara nyingi.
2) Ilionekana kifaa
cha mambo ya umeme (circuit breaker) chenye capacity ya 180 A brand ya ABB
ambacho kinatakiwa kufungwa kwenye mfumo wa umeme wa motor hiyo pia hakipo, na
kilitakiwa kuwagizwa aidha Musoma au kuingine; hii ni baada ya mkandarasi
kuwambia kuwa amekituma kwa ndege toka arusha kuja seronera na baada ya kufika
seronera kwa bahati mbaya tena ndege imerudi nacho arusha baada ya kukosewa
jina la mpokeaji.
3) Tatu, ilikuwa tu ni
vifaa vingine vidogo vidogo vilivyoshauriwa na mtaalam toka wizani kuwa ni
vyema vikafungwa hapo ili kukomesha tatizo hilo kujirudia hasa katika mfumo wa
umeme, vitu ambavyo pia inaonekana vinahitaji fungu Fulani ili kuletwa.
Katika
mahojiano ya hapa na pale, ilionekana kuwa Mkurugenzi wa MUWASA ndiye anapaswa
kumbana mkandarasi kwani MUWASA ndiyo iliyosaini mkataba na mkandarasi. Akiongea
kwa masikitiko mwakilishi wa wizara ya maji (jina halikupatikana) amesema,
MUWASA ni mamlaka kamili, hivyo wao kama wizara wanakosa nguvu ya kuingilia
jambo hilo na kumforce mkandarasi, ila watajaribu kumshauri MUWASA kuona namna
ya kumbana supplier ili afike mapema badala ya hiyo anayosema jumatano; na timu
yake ya wizara haitondoka mpaka tatizo limekuwa solved; huku akihofia kuwa
endapo itafika sept. 06 kabla ya maji kutoka, kuna hatari ya waziri wa maji
kupata wakati mgumu bungeni toka kwa Mbunge wa Serengeti.
Pamoja
na mambo mengine, watalamu wa wizara na Muwasa pia kila mmoja wameonyesha
kushangaa jinsi wanamugumu walivyo kimya huku wakiwa na tatizo kubwa kama hili. Mmoja wao
amesema yeye alikusudia angefika akakuta (Nyomi ya watu) yaani kundi kubwa la
wananchi wakiwa bwawani kama sehemu ya kudai kupata huduma ya maji, kama
alivyowahi kushuhudia katika miji mingine aliowahi kufika kwa kesi kama hii. “Miezi
4 bila maji sii jambo dogo”, alisema. Mpaka mwandishi wetu anaondoka eneo la
tukio, motor haikufungwa na kila mmoja alionekana kumtupia lawama supplier na
mafundi wote wa muwasa na wizara wameondoka kuridi musoma hadi siku
watakapofika mafundi wa supplier.
==Mwisho==
| Kazi inaendelea. |
| Gari ya MUWASA iliokuja na mafundi wa MUWASA na wale wa kutoka wizara ya maji (dsm) |
| Baada ya zoezi kuahirishwa, kazi ikawa ni kurudisha motor stoo |
| Makatibu wote wawili wa Mbunge, wa kiwasaidia mafundi kurudisha motor stoo, inaonekana ndogo ila ina uzito karibu 300kg |
